
Nakusihi kama wewe ni BOUNCER💪 wala usijiandae kumdhoofisha aliye na PENDO LA DHATI💑
Bora nguvu hizo ukaponde kokoto ZINALIPA sana tu, Kama wewe unazo pesa💸💵💴💶💷💰 na uko tayari kupigania PENZI kwa thamani ya pesa huku kuna mtu analo pendo la dhati huko unakokulilia MY FRIEND PESA HIZO KALIMIE TIKITI🍉 UTAVUNA UUZE UPATE FAIDA🙋
Lakini nikwambie tena kama kuna kitu hupashwi kugombania ni PENZI maana nijuavyo mimi HUWEZI KUSHINDA MBIO🚴🚴 ZA MAPENZI ikiwa utashindana na na mtu ambaye yeye anatumia NGUVU YA UPENDO WA DHATI halafu wewe unatumia nguvu ya dawa💊 na makadharika mazee utapata taabu mno😅😅Mwenye UPENDO kapewa kibali cha kukubaliwa wakati wewe hunacho, Pengine yupo ambaye nae ameandikwa kwa maisha yako hivyo USIPARAMIE ASIYEKUWA WAKO huyo atakutesa mno😭 Wacha UPENDO WA DHATI USHINDE ili unafiki uzidi kutokomea ili KAMA KUNA MWENYE UPENDO WA DHATI AENDELEE KUFAIDI MATUNDA YA PENDO LAKE💃 Upendo unalipa rafiki KOMAA💪