-->

FAIDA ZA KUKUMBATIANA

UTAMU KITANDANI APP
Mwanandoa mmoja aliulizwa unajuaje kua mume wako anakupenda sana? Akasema" Anapenda kunikumbatia mara kwa mara zaidi ya mara sita kwa siku, akiingia akitoka akilala,akiamka ,akiwa na furaha akiwa na huzuni, na kuna mda anaponiona nimetingwa na kazi ananiambia ninatamani kumbatio lako honey wangu,nami ninaacha niliyonayo tunakumbatiana....mara nyingi tunaongea huku tukiwa tumekumbatiana....hili ni jambo linalonifurahisha sana na kuona ni jinsi gani ananipenda pamoja na kua ninapomkwaza hanikumbatii hadi nimuombe radhi ..."
1. Kumbatio linastawisha mahaba.
2. Kumbatio linamaanisha mmesameheana na kila mmoja yuko radhi na mwenzake.
3.Kumbatio linamaanisha kufungua ukurasa mpya.
4.Kumbatio linajenga umoja na mshikamano.
5.Kumbatio linatuliza moyo .
6. Kumbatio linamfanya kila mmoja ajiskie yuko salama kwenye mikono salama.
7. Kumbatio linaliwaza na kuamsha hisia za upendo wa dhati.
8.Kumbatio linamfariji mmoja wapo anapokua na huzuni.
9.Kumbatio ni kuonesha kimatendo kua nyinyi ni kama nafsi moja mwili mmoja.
10.Kumbatio linajenga ndoa iwe na furaha isiomalizika.
Usichoke kumkumbatia mume wako/ mke wako.
Kama ulikuwa hujui faida ya kumkumbatia Mume/Mke wako sasa tayari nadhani kushajuwa sasa kama mulikuwa hamna hii tabia nakushauri uwanze sasa
Mw.Mungu atufanyie wepesi inshaallah
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU