-->

ULISHAWAHI KUJIULIZA KWANINI MWANAMKE ANALIA KIRAHISI ANAPOUMIZWA!

UTAMU KITANDANI APP

Kaka👇👇
Ushawahi kujiuliza kwanini mwanamke analia kirahisi anapoumizwa? Ni kwa sababu mwanamke hapendi matatizo. Pale alipo mwanamke, hua panakua na mpangilio mzuri ikiwemo na amani.

Muulize mtu yoyoye aliyefanikiwa, aidha atakwambia ni kwa sababu ya mama yake kumpa support au mke wake.

Mwanamke aliumbwa kuleta amani na mpangilio katika maisha. Hivyo kama sehemu hakuna amani na mpangilio mzuri mwanamke hawi comfortable hata kidogo.

Anaweza akaingia kwenye nyumba ambayo ni chafu na haina mpangilio akaisafisha na kuiweka katika hali nzuri. Anaweza akamuona mwanaume wake mchafu, asie na mpangilio wowote wa maisha akajitahidi kuyaweka maisha yake kwenye hali nzuri ingawa atakutana na vikwazo kutoka kwa mwanaume huyo ikiwemo kutosikilizwa ushauri wake.

Mwanamke anafanya kazi yake vizuri mahali ambapo kuna mazingira ya amani na mpangilio mzuri.

Kutokana na hayo, hata kwenye MAHUSIANO, mwanamke anahitaji amani na hujitahidi kwa kila hali kuwe na amani. Ukiwa kama mwanaume, ni jukumu lako kutengeneza mazingira ya amani kwa ajili ya mwanamke wako. Hautakuja kuona uwezo wa mwanamke wako katika mazingira ambayo hayana amani.

Anapokuwa hana amani na wewe, mwanamke wako hujisikia hawezi kitu, ile nguvu yake ya ndani haiwezi kuonekana, ule uwezo wa usaidizi humpotea kabisa.

Kama ukitaka kumfaidi mwanamke wako, mpe amani, mjali na mpe ile attention anayoihitaji. Kuwa karibu yake pale anapokuhitaji msikilize huku ukimuangalia machoni mwake,mwambie ndio maana nakupenda

Mwanamke anapokua na amani, uhakika na kujiamini kwamba yupo sehemu sahihi, ile nguvu na uwezo wake huja automatically. Atakuombea mara kwa mara wakati ukihangaika kujitafutia kipato. Usitegemee mwanamke akuombee ufanikiwe wakati mafanikio yako ni mwiba kwake.

Unapomjali vizuri mwanamke wako alie bora, atakupa support ambayo hauwezi kuitegemea. Mungu husikia kilio cha wanawake. Mungu hujibu maombi ya wanawake.
Ndio maana kuna wanaume wengi leo toka wameaanza kutafuta maisha hawajafanikiwa ila siku tu wakiamua kuchagua mwanamke na kuoa wanatajirika
@maisha_halisitz
Zaidi njoo lipia ushauri ni elfu 10 tu
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU