-->

UNAJUA KWA NINI MPENZI WAKO HASHINDI NYUMBANI!?


Hakuna kitu kidogo ila kizuri kinachopendwa na wapenzi hasa wa kike kama mpenzi, mchumba au mume wake kushinda nyumbani siku za mapumziko, wanawake wanapenda sana wanapenda, kupita mbele ya wenza wao ili wawaone walivyobarikiwa, wanapenda sana angalau kupata muda wa kuzungumzia maendeleo ya familia yao japo kwa siku moja.


Kwa kufanya hivyo hakika nakuambia utakuwa umeongeza umechachuza sehemu ya penzi lenu kulifanya lionekane angavu tena kwa mar nyingine. Ebu jaribu, tena sio kujaribu badilika na anza kushinda nyumbani na familia yako siku ya mapumziko hata watoto wanakuhitaji kama baba yao, hata mifugo yenu kama ng’ombe nao wanafurahi wakikuona mara moja moja.

Sio kweli kwamba wanaume wote hawapendi kushinda nyumbani, lah hasa wapo wengine wanapenda kabisa ila kutokana na tabia ya mwenza wake inamfanya aamue kutokushinda nyumbani na kwenda kwa rafiki zake ama bar kula masanga ili akirudi nyumbani muda wa marumbano na vijembe uwe angalau umepungua kidogo.

Ushauri wangu angalia na rekebisha mapito yako, jiulize nini ni kero au karaha yako inayomfanya mumeo, mchumba au mpenzi wako asishinde nyumbani, au ni ile tabia yako ya kidomodomo, au ni ile gubu yako
Wakati mwingine mwenza wako anaamua kutokushinda ndani kwasababu tu anajua akishindanawe ndani siku haitaisha bila kuzinguana, bila kutukanana au kushikana singilendi na kadhalika.

Sio kweli kwamba wote wanakuwa na mambo yao wengine wanakimbia kero kerom zenu. Ingawa pia kuna wengine wanatumia fursa hiyo kama njia ya kuchepuka kwa maana ya kuondoa stesi za makelele yako.
Na wewe mwanaumea anza kurekebisha tabia zako pengine ndizo zinamfanya mwenza wako aanza kukukulalamikia nahata kukwidana naye, yawezekana wewe pia ndiyo sababu ndiyo chanzo. Kama utaweza kurekebisha suala hilo utakuwa umitendea haki familia, mkeo, mpenzi na hata nyumba yako.

Mapenzi bhana umiza kichwa. Tukutane kwenye mada nyingine.
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU