ποΈUkweli ni kwamba NDOA haikimbiwi, ukiingia umeingia, NDOA ni kama mfano maji uliyoyavulia nguo kwa maana utayaooga tu ikiwa tayari upo kwenye Ndoa ni kuendelea tu. Pale unapoona watu ambao ni Wazee kwenye NDOA ujue kuna mengi wamepitia ndio maana hata sasa bado wakidunda.
ποΈUkifanikiwa kuongea na Mwanandoa mkongwe atakueleza siri zilizowafanya kufikia umri huo wa Ndoa.
ποΈ Lakini Ndoa si Ndoa bali Ndoa yenye kujengwa kwenye msingi imara wa Mungu hiyo ndio NDOA ninayoizungumzia hapa.
ποΈ Hivyo ni vyema ujifunze siri hizi za kuinogesha NDOA yako / kuiomarisha NDOA yako ( to build a great marriage).
βοΈSiri zipo nyingi, lakini siri zote zimefungwa kwenye neno moja, nalo ni;
β€οΈUpendo.
βMsiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.β Warumi 13:8-10
βMsiwiwe na mtu cho chote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria.Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.β Warumi 13:8-10
βοΈNeno linaeleza kwamba, usisumbuliwe na mambo mengine yoyote isipokuwa kupenda tu. Kwenye NDOA ni vivyo hivyo, usisumbukie kutengeneza sheria ili Ndoa yako iwe sawa, bali wewe PENDA tu/ PENDO lako la dhati li juu ya sheria zote. Kwa sababu ukipenda hutakubali kumuumiza mpenzi Mume/Mke wako, hutakubali kumsononesha Mpenzi Mume/Mke wako, hutakubali kumpiga, hutakubali kumfanyia hila nakadhalika. Ukweli ni kwamba ;Ukimpenda Mumeo ujue umeitimiza sheria na Mumeo ni vivyo hivyo. Kwa maana hutaitajika kuambiwa βusinzini, usiue, usitamani, na amri nyingine yoyoteβ bali ukipenda moja kwa moja huwezi kumwibia mwenzako penzi lake na kushea na mtu mwingine, tena huwezi kutamani nakadhalika.
βοΈKumbuka Pendo halimfanyii jirani ( mpenzi wako Mume/Mke) neno baya, kwa kuwa pendo ndilo utimilifu wa sheria.
βοΈUmeshawahi kuona mtu anampenda mwandani wake kuliko ajipendavyo mwenyeweβ Ndio wapo watu wa namna hii. Je unafikiri mtu wa namna hii, kweli ataweza kumsononesha, kumpiga au kumtenda mambo ya hiyana mwandani wakeβ Jibu ni hapana, hawezi kuthubutu kumfanyia ujinga mwenzake.
βοΈ Kumbe shida ya ndoa yako ni kukosekana kwa pendo halisi, na huo ndio ukweli.
βοΈMatokeo ya kukosekana kwa pendo la kweli ndani ya NDOA ndio tunayaona magomvi yasiyoisha, chuki, adhabu ya kunyimana unyumba, kelele na matukano yasiyoisha, mauaji nakadhalika
βοΈBiblia inasema ββ¦ Pendo ndilo utimilifu wa sheria βikiwa na maana hakuna sheria yoyote itakayosimama kwa mwenye pendo. Huwezi kumwambia Mkeo / Mumeo β kuwa Mwaminifu β bali akipenda / akiwa ndani ya pendo ni lazima atakuwa mwaminifu kwako.
βοΈ Ssasa umegundua shida iliyopoβ Ni moja tu, βPENDO halipo kwenye ndoaβ na PENDO sio tendo la ndoa, au kumshikashika Mumeo hadi waambiwa usimshike atakuwa "malinda "huo sio UKWELI kwa mtazamo wangu π naona si vema kuwafundisha Wanawake Mawazo hayo potofu , useme kwamba β kwa sababu ninampa Mume wangu kila wakati akihitaji, hivyo nampenda , sio sex yenye kupima UPENDO β€οΈβ ( na Mume ni vivyo hivyo sio mabao ya nguvu unayomfunga Mkeo ndio UPENDO β€οΈ). PENDO ni zaidi ya tendo la ndoaβ Ingawa β PENDO β ndio mworobaini / dawa yenyewe ya kuboresha NDOA yako, lakini ni vyema nikuchambulie moja moja ambalo litaboresha au kujenga ndoa yako kuwa ndoa babu kubwa! Nayo ni ;
Mweshimu MUME/MKE
βοΈNaliwaona Wanandoa fulani ambao kwa kweli hawaeshimiani hata kidogo.
βοΈNa kwa sababu hiyo Ndoa ilikuwa chungu badala ya kuwa tamu.
βοΈ Mume alimdharau Mkewe na Mke naye akamdharau Mumewe. Ilikuwa ni hivi;ππ π Mwanaume anamwita Mkewe maneno ya ajabu ajabu, Mwanaume anawakumbuka Wanawake zake wa zamani aliokuwa nao, akifikiri kwamba walikuwa wakimweshimu sasa bahati mbaya amejisahau kwamba Yeye sasa ni Mume wa mtu na ameokoka.
βοΈ Mke wake baada ya kuona dharau zimezidi, naye β akamtupa kapuniβ ( hakumjali kwa lolote) Jamani, waswahili wanasema ;
βοΈβ Heshima ni kitu cha bure, haiuzwi! β jifunze kumheshimu mwandani wako katika mambo yote.
βοΈ Jukumu la β heshima ndani ya Ndoa β sio suala la mtu mmoja tu. Bali kila mmoja na ajifunze kumweshimu mwenzake. Mara nyingi katika utamaduni wetu wa kiafrika tunakosea, kwa maana tumekuwa na mtazamo mbaya juu ya neno βheshimaβ tukidhani kuwa heshima ni kutii. Na tunafikiri Mke ni lazima amweshimu Mumewe na hatujui kwamba na Mume anapaswa amweshimu Mkewe. Heshima sio utii, bali ni hali ya kumtanguliza mtu kuwa anafaa zaidi.
Hakikisha UNAWAACHA WAZAZI / WALEZI.
βοΈSiku moja, Wanandoa fulani walikuwa na mpango wa kununua shamba eneo fulani hivi, wakawa na mpango wa kujenga pia.
βοΈMipango hii ilikuwa ni ya Wanandoa hao. Lakini Mwanaume alikuwa na desturi ya kumuuliza Mama yake katika yote waliyopanga na Mkewe.
βοΈSasa akamwuuliza β Mama mimi na mwenzangu tunataka kununua shamba na maeneo hayo hayo tujenge huko β Mama yake alikataa hayo maamuzi yao β hapana sitaki mwende kujenga huko, wala hamna sababu ya kujenga kwa sasa, nitawaambia muda sahihi wa kujengaβ¦ β
βοΈBπasi yule kijana, akatoka hapo na maamuzi ya Mama yake. Alipofika kwa Mke wake, akapangua mipango yao.
βοΈπππ Sasa hali hii iliwasumbua sana hata kupelekea magomvi ndani ya Ndoa yao. Je unafikiri huyu Mwanaume amewaacha Wazazi wake kweliβ
βοΈ Hapana bado yupo na Wazazi wake kwenye Ndoaβ
βοΈ Ni kweli Wazazi wanasehemu yao muhimu sana kwenye Ndoa, wao wameyaona mengi hata wakati mwingine wakikushauri yafaa kabisa kufanya hivyo.
βοΈLakini isiwe kwamba mamlaka ya kimaamuzi yatoke kwao, hapo ndipo kuna makosa.π
βοΈWazazi wakiwa ndio wasemaji wa mwisho katika mipango yenu, ujue ilo ni tatizo baya sana. Ili uweze kuijenga imara Ndoa yako yakupasa uwaache Wazazi, na uhakikishe maamuzi, mipango, mambo yenu yanabakia ya kwenu kwenu isipokuwa pale tu inapobidi kuomba msaada zaidi kwa Wazazi iwe hivyo.
βοΈ Baba na Mama yako na wenyewe wanayakwao, na isikute yakwao yenyewe yanawashindaβ
βοΈWao ni Wazazi na sehemu yao ipo pale pale, lakini isizidi ya hapo.
βοΈ Hujawahi kuona mtu akigombana na Mpenzi β€οΈ Mume π/Mkeπ wake kwa sababu Mzazi ameingia sana kwa mambo ya Watotoβ
βοΈ Ndio zipo ndoa zinazopitia majanga kwa sababu mmoja hajaamua kuwaacha Wazazi wake.
βοΈ Ebu jihoji jambo hili kwenye Ndoa yako limekaajeβ Je wewe upo sawaβ Au Mpenzi β€οΈ Mume/Mke wako je amefaulu kuwaacha Wazazi / Walezi au jamaa zake wakaribuβ
βοΈWakati mwingine sio Wazazi tu, hata ndugu au jamaa zako wa karibu kama Marafiki, hao wote hawapaswi kuwa wenye sauti kwenye Ndoa yenu.
βοΈ Hujawahi ona jinsi ambavyo marafiki wanavyochangia kuharibu ndoaβ
βοΈ Ni kweli marafiki wanaweza kuchangia vizuri kuijenga Ndoa yako, lakini sehemu kubwa ya mchango wa marafiki ni kubomoa na sio kuijenga Ndoa.
βοΈSasa angalia kile utakachopanga au kujadili na Mpenzi β€οΈ Mume/Mke wako, alafu pembeni awepo rafiki ambaye wewe humjui lakini kinyemela yupo pamoja na Mpenzi β€οΈ Mume/Mke wako huko wanapokutana.
βοΈAngalia tabia ya Mpenzi β€οΈ Mume/Mke wako itakavyokuwa, angalia mipango yenu itakavyokuwa, alafu uniambie kama mambo hajaenda komboβ
βοΈIfike wakati sasa, uachane wale wa nje ambao wamekuwa na nafasi ya kushauri mambo ya Ndoa yako na wakitaka ufanye hivyo.
βοΈ Ndoa ni ya kwako na mpenzi / Mwanandoa wako. Usipoweza kuwaacha Wazazi kwenye fikra zako, ujue Ndoa π haitaweza kuimarika.
βοΈFanya maamuzi leo kwamba maamuzi yenu yaendeshwe na ninyi wenyeweβ¦π
NDOA π NA IHESHIMIWE NA watu WOTE NA MALAZI YAWE SAFI π MAANA waasherati na wazinzi MUNGU ATAWAHUKUMIA adhabu (Waebrania 13:4)