Karibuni katika mada yetu mpya ya leo. Kwa mujibu wa vitabu vya dini, vinatufundisha kwamba kiasili mwanaume ndiye kichwa cha familia. Ndiye anayepaswa kusimamia maamuzi yote ya familia sambamba na suala la fedha.ππππππππππππππππππππ
Mwanaume ndiye anayetoa fedha kwa watoto, ndiye anayempa mkewe fedha kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Huo ni utaratibu tu uliozoeleka, leo nataka nikujuze kwamba si mzuri sana.ππππππππππππππππππππ
Kwa kutumia falsafa hiyo, wanawake wengi wamekuwa wakiwategemea wanaume kwa kila kitu. Wanabweteka. Wao wanategemea kila kitu kupewa.ππππππππππππππππππππ
Utasikia ‘baba fulani nataka niende saluni naomba hela, baba nanii naomba hela kwa ajili ya mchezo au nipatie fedha za kununulia nguo za mtoto’.ππππππππππππππππππππ
Kautaratibu haka kamewakaa hata wanaume. Wengi wao huwa hawana kipingamizi waombwapo matumizi ya kila kitu, wanatoa hata bila ya kuhoji mkewe anafanya kazi ambayo inamuingizia kipato au la.ππππππππππππππππππππ
Mbali na kwa wanandoa, dhana hii imejengeka hadi kwa wachumba. Mabinti wengi wanaoingia kwenye uchumba kwa kizazi cha sasa wanaamini katika falsafa ya kuhongwa. ππππππππππππππππππππ
Wanataka kila kitu kutoka kwa mwanaume hata kama na yeye ana kazi yake. Hiyo haimhusu mumewe, ‘cha mumewe ni cha kwao, cha kwake ni cha kwake’.ππππππππππππππππππππ
Wanaomba fedha za vocha, wanaomba fedha za matumizi ya nyumbani na hata zile za kuendea saluni pia. Anahakikisha mchumba wake anakuwa ndiyo ‘injini’ ya kutoa kila kitu.ππππππππππππππππππππ
Na endapo ikitokea siku ameomba fedha za kitu fulani akanyimwa basi ni tatizo. Ugomvi ndiyo unaanzia hapo.ππππππππππππππππππππ
Atakasirika na kuanza kumuondoa thamani mpenzi wake. Ni rahisi kwenda mbali na kufikia hatua ya kusema ‘huyu mwanaume hana sifa za kuwa na mimi. Mwanaume gani anashindwa kunilipia hela ya saluni. Mwanaume suruali.’πππππππππππππππππππππ
Ugomvi utakuwa mkubwa na suluhu yake huwa ni kuhamia kwa mwanaume mwingine ambaye atakuwa hazisikilizii fedha zake.ππππππππππππππππ
Tabia huwa ni kama ngozi, huwezi kuibadili. Utakutana na mwanaume mwingine ambaye naye ana fedha, lakini pale atakapoyumba kiuchumi tu, naye utamuacha na kutafuta mwingine.πππππππππππππππππ
Staili ya maisha yako itakuwa ni ya kutanga tanga. Leo kwa huyu kesho kwa mwingine.πππππππππππππ
Tatizo hili pia lipo hata kwa wanaume. Wapo ambao nao wanaamini katika falsafa ya kuhongwa na wanawake.ππππππππππππ
Hawataki kujishughulisha, wanataka kuhongwa. Mwanamke asipomhonga naye hamtaki, anatafuta mwingine ambaye ataweza kumtimizia mahitaji yake yote. Kama ana kazi yeye mshahara wake unakuwa na matumizi yake ambayo anayajua mwenyewe.ππππππππππππππππππππ
*Ndugu zangu lazima tukubaliane kwamba katika ulimwengu wa wapendanao fedha zinachangia kurahisisha maisha lakini zinageuka kuwa tatizo pale mnapozipa kipaumbele kwenye uhusiano wenu. Kwamba fedha ikitoweka na uhusiano umekufa*.πππππππππππππ
Maisha ya uchumba na hata ya ndoa yanapaswa kukubaliana na hali halisi mliyonayo. Kama mumeo ana kazi na wewe huna kazi, kwa kizazi cha sasa kinakupasa na wewe kubuni vimiradi vidogovidogo ambavyo vitampunguzia makali ya maisha mumeo.πππππππππππππππ
Itakusaidia kuondoa tatizo la utegemezi katika kila kitu. Maisha ni kusaidiana, ondokana na tafsiri ya kusema mwanaume ndiyo kichwa basi umtegemee kwa kila kitu. Vingine unapaswa ujiongeze wewe mwenyewe, hiki si kizazi cha mwanandoa kuwa golikipa.ππππππππππππππππππππ
*Wanaume ambao pia wana kamchezo haka wanatakiwa kubadilika. Huwezi kumtegemea mwanamke awe anakupa wewe fedha kila siku. Jengeni utaratibu wa kusaidiana lakini si kila siku mmoja tu ndiye awe anaumia*πππππππππππππππππππ π