-->

Mwanamke akipenda anapenda kweli!


No photo description available.
Mwanamke akikupenda anakuwa na furaha, anakuwa anajivunia kuwa na wewe, na hujihisi furaha kuongea na wewe.

Hupenda awe rafiki wa rafiki zako na ndugu zako, uvipendavyo na yeye atavipenda, atabadilisha mtindo wake wa maisha kuendana na mtindo wako.

Haitajalisha ni kiasi gani utamuudhi, atakusamehe hata kabla hujamuomba msamaha, atachokifanya ni kusubiri tu umuombe msamaha kuthibitisha kama kweli umejutia kosa lako.

Atajaribu kuwa na wivu na atakulinda kwani atahitaji uwe wake, wake peke yake na sio ku share. Atawakataa wengine wote wanaomtongoza kwa sababu ameona kesho yake ipo mikononi mwako.

Haitajalisha ni kiasi gani uko mbali na yeye, atajilinda kwa ajili yako. Atalike na ku comment kila kitu unachoweka facebook hata kama ni cha kipuuzi (hahaahaa).

Atakujibu kwa wakati text zako either watsapp, za kawaida au inbox ya fb. Hatajali kama unampa pesa au laa, kama ni tajiri au laa kwa sababu lengo lake ni kujenga maisha na wewe na sio kupass time ameona potentials kwako.

Atakuonyesha marafiki zake na ndugu zake, kwa sababu anajivunia kuwa mpenzi wako.

Tafadhali sana, muangalie mwanamke huyo, moyo wake umejawa na mapenzi, anastahili kutunzwa na kupendwa kama almasi.

Lakini tatizo kubwa la hawa "wavulana" (baadhi yao) baada ya kumfanya akupende zaidi, baada ya kupoteza muda wake juu yako, baada ya kuwakataa wanaume wengine ambapo kimsingi wengine walikuwa tayari kumuoa, baada ya kumuacha akutambulishe kwa ndugu zake na marafiki sasa unamuacha, unamkataa kwa mbwembwe nyingi, unamuacha akiwa na maumivu na aibu kubwa kwamba atawaambia nini wazazi wake, ndugu na marafiki, atatambulisha wangapi?

Na akiulizwa yuko wapi yule uliyetutambulisha? Awajibu nini!? Ofcoz atakachofanya ni kuinamisha kichwa huku ameshika mashavu! Hana jibu ni aibu na maumivu makubwa kwa kuwa alikupenda kwa dhati.

Mbona mnawaweka katika wakati mgumu wanawake waliopewa moyo wa kupenda?

Brothers, usimfanye mwanamke wako ajute kwanini alipenda, usifanye wengine wamcheke na kumdhihaki. Timiza ahadi yako, kama amekukosea na kukuomba msamaha jaribu kumpa nafasi ya pili. Kila mtu anahitaji nafasi ya pili ili aweze kurekebisha pale alipokosea.

Na nyie vijamaa mnaokua sasa, miaka 14 na kuendelea msiige tabia ya sisi kaka zenu, hiyo sio tabia njema kabisa. Jifunzeni kuheshimu hisia za mtu. Kujeruhiwa kihisia kunauma kuliko maumivu ya risasi.

Kama huna future nae usimtongoze na kumpa mimba.

I CARE.
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU