-->

USHAURI KWA WANAUME WOTE


NDOA SIO MCHEZO
Kama unafikri ndoa ni sherehe unakosea wewe bado mtoto..😍😍
Kama unafikiri jinsi utakavyo tokelezea na kushine na mke/mme siku ya harusi wewe bado mdogo, waachie wakubwa ..😍😍
Ikiwa wafikri jinsi ukumbi utavyojaa na watu kucheza wewe u bado kinda, waachie wakubwa ..😍😍
Ikiwa bado wafikri na kuwaza namna mtavyokula keki, vyakula na kunywa kwa shangwe, u mtoto wewe waachie wakubwa..😍😍
Ikiwa bado unafikri zawadi, pesa na vitu vya thamani utakavyo pewa hujakua wewe u mtoto, waachie wakubwa...😍😍
Bado unafikiri marafiki watakavyo jaa na kupongeza na kukusifu tambua bado hujakuaa😍😍
Ikiwa bado wawaza jinsi mama baba kaka dada na ndugu watakavyokusifu kuwa umechagua, hb au beautiful spouse jiweke kwenye kundi la watoto, ndoa waachie wakubwa😘😘
Ndoa inaanza baada ya kubaki wawili, wakisha ondoka wengine wote ...mnabaki wawili mume na mke,hapo ndio ndoa inaanza..ndio maisha yanaanza, ndiyo dhana ya ndoa inaanza..👫💑
Sherehe ya ndoa ni siku moja tu..ni masaa machache tu na ni furaha ya masaa tu. Yakiisha haya masaa yanafuata maisha, maisha ya ndoa. Maisha ya ndoa yana ugumu wake, yana raha yake...🙅🙅
Unahitaji kujua thamani ya maisha iliyo katika ndoa ...
Thamani ya kuvumiliana🙋
Thamani ya msamaha🙇
Thamani ya kupendana💓
Thamani ya kushirkiana na kushirikishana💏
Thamani ya kuwa mwili mmoja, mtu mmoja
Thamani ya kukubali kuacha anasa zote na kuishi maisha ya ndoa...
Sir Franko Samue
Share...
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU