-->

UNAFIKIRI NI KWANINI WANAWAKE HUPENDA MAPENZI YA UWAZI?

 
Image may contain: 2 people, people smiling

Mara nyingi wanaume huwaficha ndani wapenzi wao ama wake zao ili kuzilinda tabia zao za michepuko, Kila mwanamke timamu akitongozwa na mwanaume lazima aulize JE HUNA MPENZI? Na majibu ya wanaume wengi hujibu NDIYO... Kitu ambacho humpa nafasi mwanamke kumfikiria mwanaume huyo, Wanawake wamejaaliwa akili za tofauti sana dhidi yetu wanaume na ndo maana hata watoto mapacha wakiwa jinsia mbili yaani wakike na wakiume anayeanza kutambaa wakike, anayeanza kuongea wakike hilo sio Mimi nimesema ila ndo MUNGU alipanga iwe hivyo, Ila sijui wapi wanawake walinyimwa kubaini mitego ya wanaume ama laaa ni ule udhaifu wao wa tangu wanaumbwa! Unakuta ndoa watu wanapendana sana na kila mmoja anafurahia uwepo wa mwenzi wake lakini HAWANA SAFARI WALA MITOKO YA PAMOJA na tabia hii iko zaidi kwa wanaume kuliko wanawake, Ni wanawake wachache ambao huwaficha waume zao Kwani fahari ya Mwanamke ni kuwa na Mume, Mwanamke mpaka amkubari mwanaume anakuwa ameamua kwa lolote, Wanawake walio wengi hupenda kuambatana na wapenzi wao au waume zao ili kutengeneza ulinzi katika ndoa ama mahusiano yao Kwani wanawake walio wengi hawapendi mwanaume aliye na mke au aliye katika mahusiano japo kumpata mwanaume huyo ni MPAKA MITUME WA ZAMANI WARUDI! Maana kila mwanaume anaye mwanamke wake na kama ukikuta mwanaume hana mwanamke ujue ana tatizo aidha la ugonjwa au amegundulika tabia zake hivyo vimwana wanamkwepa... HIVYO UKIONA HAPENDI KUTOKA NAWE UJUE WAKO WENZIO ANAWAOGOPA.
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU