-->

NJIA ZAKUACHA KUFIKIRIA NGONO MUMEO AKIWA MBALI



“MIMI hujikuta nikifikiria wasichana saa zote—hata wakati ambapo hawapo,” asema kijana mmoja anayeitwa Michael. “Sielewi. Nyakati nyingine siwezi kukazia fikira jambo lolote!” Je, wewe hutumia saa nyingi ukiwaza juu ya watu wa jinsia tofauti, kama anavyofanya Michael? Ikiwa ndivyo, huenda ukahisi kana kwamba unapigana vita na akili yako. Fikira za ngon-o huingia akilini mwako kama jeshi la adui. “Fikira hizo zinaweza kukutawala,” asema Michael. “Zinaweza kukufanya uzunguke njia ndefu ili tu umtupie jicho msichana fulani mrembo, au kutembea-tembea dukani wakati ambapo hukusudii kununua chochote ili tu umtazame mtu fulani kwa ukaribu.” Hata hivyo, kumbuka kwamba kuwa na hisia za ngo-no si dhambi. Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wakiwa na uvutano wenye nguvu kati yao, na hakuna ubaya wa kutosheleza tamaa za ngo-no katika mpango wa ndoa. Kabla ya kufunga ndoa, huenda ukawa na tamaa kali za ngo-no. Hilo likitokea, usidhani kwamba wewe ni mtu mwovu au kwamba huwezi kuishi maisha safi. Unaweza kudumisha usafi wa kiadili ukiamua kufanya hivyo! Lakini ili ufanikiwe, utahitaji kudhibiti mawazo yako kuhusu watu wa jinsi tofauti. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani? Angalia watu unaoshirikiana nao. Wanafunzi wenzako wakianza kuzungumzia mambo ya ngo-no, huenda ukataka kuchangia mazungumzo hayo—ili tu usionekane mshamba. Hata hivyo, kwa kweli kushiriki mazungumzo hayo kutafanya iwe vigumu zaidi kwako kudhibiti mawazo yako. Ufanye nini? Usimame tu na kuondoka? Ndiyo, na usione aibu kufanya hivyo! Mara nyingi inawezekana kuondoka pasipo kuonekana “mtakatifu” au kuwafanya wenzako wakucheke. Epuka kujifurahisha kwa mambo machafu. Bila shaka, haimaanishi kwamba sinema zote, au miziki yote ni mibaya. Hata hivyo, katika ulimwengu wa leo burudani nyingi zimekusudiwa kuamsha tamaa zisizofaa za ngo-no. Biblia inatoa shauri gani? “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1) Epuka kabisa burudani zote zinazoweza kuchochea tamaa zisizofaa za ngo-no.* Tatizo la Kupiga Puny-eto Vijana fulani hujaribu kupunguza tamaa ya ng-ono kwa kupiga puny-eto. Lakini kufanya hivyo kunaweza kutokeza matatizo makubwa. Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngo-no, tamaa yenye madhara, na kutamani.” (Wakolosai 3:5) Kupiga puny-eto ni kinyume kabisa cha ‘kuua hamu ya ngo-no.’ Kwa kweli, kupiga punye-to huchochea na kukuza hamu hiyo! Kupiga punye-to kwaweza kukufanya kuwa mtumwa wa tamaa zako. (Tito 3:3) Hatua moja unayoweza kuchukua ili kushinda zoea hilo ni kuzungumza na mtu unayemtumaini. Mkristo aliyekuwa na tatizo la kupiga puny-eto kwa miaka mingi anasema hivi: “Laiti ningeweza kupata ujasiri wa kuzungumza na mtu fulani kuhusu tatizo hilo nilipokuwa kijana! Kwa miaka mingi nilisumbuliwa na hisia za hatia, nazo ziliathiri sana uhusiano wangu na wengine, na zaidi ya yote, uhusiano wangu na Yehova.” Ni nani unayeweza kuongea naye? Mara nyingi ingefaa kuzungumza na mzazi. Au huenda Mkristo mkomavu kutanikoni anaweza kukusaidia. Unaweza kuanza kwa kusema, “Ningependa kuzungumza nawe kuhusu tatizo linalonisumbua sana.” André aliongea na mzee Mkristo, naye anafurahi kwamba alifanya hivyo. “Mzee huyo alipokuwa akinisikiliza, alilengwa-lengwa na machozi,” André anasema. “Nilipomaliza kuzungumza, alinihakikishia kwamba Yehova ananipenda. Aliniambia kwamba watu wengi wana tatizo kama langu. Aliahidi kwamba atakuwa akizungumza nami mara kwa mara kuona nimefanya maendeleo kiasi gani na kuniletea habari zaidi kutoka katika vitabu vinavyotegemea Biblia. Baada ya kuongea naye, niliazimia kupiga vita zoea hilo—hata ikiwa ningeanguka mara moja moja.” Mário aliamua kuongea na baba yake, aliyemjali sana na kuelewa hali yake. Hata alikiri mbele za Mário kwamba alipokuwa kijana haikuwa rahisi kwake kushinda zoea hilo. “Nilitiwa moyo sana na mazungumzo hayo ya waziwazi na unyoofu wa baba yangu,” asema Mário. “Nilijiambia, ikiwa al
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU