-->

JE TUNAWEZA KU SOLVE MIGOGORO NA KUEPUKA MAAFA AU MAHUSIANO/NDOA KUVUNJIKA???


Palipo na upendo wa dhati hapakosi malumbano ya hapa na pale.
Lakini kudumu katika amani kutategemeana na jinsi gani mnapambana kuyamaliza malumbano yenu.
"Kwenye mahusiano ni ngumu kuepuka malumbano yasitokee, sababu usipomchokonoa mwenzako, basi yeye atakuchonoa.
Hatuwezi yaepuka ila tunaweza epusha malumbano yasiharibu mahusiano"- Leonard Young mucky.
Mahusiano mengi yanavunjika kutokana na malumbano ya kwa mara kwa mara, na yote ni sababu.
1: Wakilumbana basi hugeuka ndio sababu ya kununiana hata mwezi mzima.
2: Malumbano mengi huwa hayatawaliwi na heshima, na huruma.
Mara nyingi mmoja hujibu kwa ukali, na kutamka maneno ya kejeli, huku mwingine akikoroma na kumsindikiza na kauli chafu au hata makofi kabisa.
3: Aliyekosea na kusababisha malumbano huwa mgumu wa kujishusha, kukubali kosa, na kuomba msamaha.
4: Aliyekosewa huwa mgumu wa kutoa msamaha, na hata akitamka "Nimekusamehe" bado hubaki amenuna na kuweka kinyongo, kujibu hovyo.
5: Mara kwa mara wanasaikolojia hushauri njia ya kuepuka malumbano yenu yasifikie pabaya hasa kwenye ugomvi. Ni kwa mmojawapo kunyamaza, au hata kuondoka eneo la tukio mpaka hasira zitakapoisha.
But in reality, kwenye mahusiano/ndoa nyingi hii imekuwa tofauti.
Katikati ya malumbano, lolote utakalojibu hugeuka ndio mada.
Mfano: Mume anasema "Umekuja hapa na kisirani chako, unaniletea mambo ya kijinga".
Mke anajibu "Kwahiyo mi mjinga, sio?"
Lolote utakalofanya hugeuka ndio mada.
Mfano: Mmegombana, kwa kuepuka hasira zisikupande, unaamua kuondoka na kurudi masaa 3 baadae.
Ukirudi unakaribishwa na mkeo kwa salamu "Nakuona ndo umetoka kwa malaya zako, sasa si bora ungelala huko huko tu tujue moja".
Kuepuka mabishano, mwanamke anaamua kunyamaza huku Mume akiwa bado anazungumza.
Mume anakasirika "Mh hivi huwa unanichukuliaje? Huu ninao ongea unauona utumbo sio? Yani me naongea na wewe, halafu unaninyamazia, haunijibu."
Tunatibu vipi hili tatizo?
Kitu nilichojifunza ni kwamba malumbano huwa yana faida kubwa sana endapo nyote mtakuwa makini na kuepuka kusababisha ugomvi mkubwa.
Iko hivi, nia na madhumuni ya malumbano kwenye mahusiano ni:
i: Kukemeana yale maovu, na yanayosababisha mnaumizana kihisia.
ii: Kufunzana lipi mwenzako hapendi ulifanye, na lipi anapenda ulifanyie.
iii: Kuongeza umakini kati yetu, mara kadhaa mkilumbana kuhusu jambo flani, na mwenzako akakukanya kuhusu jambo flani, husaidia kukuongezea umakini zaidi na kufanya mahusiano yenu yawe kwenye mstari.
iv: Husaidia kuchochea penzi, kuponya penzi lisiharibike. Sababu kulumbana kwenu husababisha kumuamsha mwenzako aliyeanza kujisahau kutimiza yanayojenga penzi.
Lakini bahati mbaya sana faida hizi huwa hatuzipati, matokeo yake tunaishia kuumizana kwa kupigana, kununiana, kuvunja mahusiano, na kujenga chuki kati yetu.
Kaa na mpenzi wako leo, na msome haya.
Fanyeni yafuatayo ili kulinda mahusiano yenu yasitetereke kutokana na malumbano tu.
1: Mapenzi ya kweli yanajengwa na huruma na upendo wa dhati.
Njia pekee ya kuepuka malumbano yasifikie pabaya, ni kwa kuepusha kutamkiana kauli mbovu.
Usitamke kauli ambayo unajua itamuumiza mwenzako, kama ilivyo nafsi yako haipendi kutukanwa, nawe usimtukane mwenzio wala kumjibu hovyo.
Hasa inaaminika, mwanamke anapohojiwa na mwanaume hatakiwi kumjibu kwa ukali, mkato mkato, wala kumtolea kejeli or kauli chafu. Sababu husababisha mwanaume kuhisi amedharauliwa na kupandisha hasira ambazo husababisha ugomvi mkubwa au maafa kabisa.
Mwanamke anapenda attention, kusikilizwa, na kujibiwa kwa heshima, kosa kubwa wanalofanya wanaume ni kujiona mwamba na kukawakatiza kwa ukali, kuwakoromea, kutowasikiliza.
Hali hii husababisha mwanamke kujihisi amedharauliwa, na kusababisha hasira kumpanda na kutamka kauli mbovu.
Haya ni mambo ambayo mwanaume unatakiwa uwe nayo makini, mjibu vizuri mkeo hata kama anakukera na maswali yake, just tumia akili kwenye majibu yako ili umuondoe dukuduku lake rohoni.
2: Huwezi dumisha mahusiano yenu kwa kujiona perfect, kwamba huwezi kukosea.
Hebu kuwa mpole unapoambiwa umekosea, jua kosa lako, na ujishushe uombe msamaha.
Kuomba msamaha sio udhaifu, bali ni dalili za akili yenye hekima na busara.
Pia tambua hakuna binadamu perfect, hata wewe una mapungufu na huwa unakosea.
Mueleweshe mwenzako usichopenda, na kuwa mwepesi wa kumsamehe.
Usimuwekee kinyongo mpenzi wako, mkiyamaliza, yaishe kabisa sio unaendelea kununa.
3: Haijalishi mmegombana, jitahidini isiwe ndo mwisho wa mazungumzo yenu.
Usimnunie mwenzio week nzima, hayo sio mapenzi.
"If you want to make a change, start with yourself. Start with the man in the mirror"- Michael Jackson.
Tabia ya kununa mwenzio atakuwa nayo, endapo na wewe unayo.
Kama hutaki hii tabia, basi jirekebishe mwenyewe Kwanza, acha kununa Muda mrefu then mrekebishe na yeye aache.
4: Mawasiliano yasikate hata kama mmegombana. Na mambo yenu msiyatoe nje, sio mmegombana kidogo tu tayari WhatsApp, mtaani, facebook, kazini wanajua.
5: Kila mtu hujiona yuko sahihi kwa upande wake sababu huwa hatuangalii tulipokosea, tunaangalia wenzetu walipokosea.
Jijudge kama hayo uliyomfanyia mwenzako ungefanyiwa ungejihisi vipi. Then jishushe.
Hasa mwanamke huwa anapenda ujishushe ukubali kosa lako, then na yeye ndo umwambie alipokosea kwa utulivu, hapo ndo atakuelewa.
6: Mwanaume kuwa romantic, baada ya malumbano mwanamke anaweza nuna au hata kutishia kuondoka.
Infact, huwa hana nia ya kuondoka wala kununa, nia yake umbembeleze tu.
Anapenda kubembelezwa hasa kwa mahaba.
7: "Mwanaume hubishana kwa point, mwanamke hubishana kwa mbinu. Ndomana ni ngumu mwanaume kumshinda mwanamke kwenye malumbano"- Deogratius Mboya (Comedian at Cheka Tu).
"Arguing with your woman is like reading software agreement, at the end you'll just click "Yes I agree" even if you don't understand."- Programmers Quotes.
Mwanaume huwezi kushindana na mwanamke kwa kubishana, hawa viumbe sio wa kubishana nao.
We tumia akili tu, mshushe presha yake Kwanza then kwa utulivu jadilini.
8: Mkifanikiwa kusolve iinshu yenu, mwanaume chukua nafasi hiyo kumbeleza mkeo, msifie sifie, mbusu busu, utamuona mwenyewe analainika na kutabasamu.
Kinachofata baada ya hapo siri yenu.
Husaidia kuongeza upendo na kutekana kihisia.
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU