-->

KWANINI USISHIRIKI PENZI LA NUSU MKATE🍞?



Hizi ndio faida za kumkumbatia mumeo/mkeo – My Blog

 Kwanza kabisa nikupe makavu pengine yatakwama kooni but ujaribu kusukumia na Mate🍟Hebu nikuulize "UNAMPENDAJE MTU AMBAYE UNAJUA TAYARI ANA MKE/MUME💑" Kwa kawaida ya UPENDO ni kwa ajili ya mmoja unaanzaje kuangukia penzi la mtu anae kupa penzi la kuiba? Sawa nakuelewa pengine unazo sababu zako juu ya penzi hilo basi yakikukuta usilalamike kwani wewe ndiye uliyepanga kuwa katika penzi hilo, Nusu mkate maana yake ni kipande utakula wewe na nusu nyingine anakula mwenzio, Huwezi kuutaja UPENDO ikiwa tayari una mtu mwingine laa ibadili sentensi yako pengine utaje UNA TAMAA! UPENDO una tabia ya kung'ang'ania ndo maana ukatajwa kwa udhaifu, Huwezi kusema UNAPENDWA NA MTU AMBAYE ANAKUGAWIA PENZI LA MWINGINE... Kataa kulishwa penzi nusu kwani unapotezewa muda bila wewe kujua madhara yake lakini fahamu jambo moja tu MUDA UNAOPOTEZA HAURUDI NA MWISHO WA YOTE NI MAJUTO🙆🏿‍♂
Share:

Popular Posts

Blog Archive

Copyright © UTAMU KITANDANIDESIGNED BY TEETOU